Friday, April 29, 2022

#VIFUU VYA NAZI.

Maajabu ya kifuu.

#vifuu ni magamba ama(fumbato) la ndani ya nazi ambayo ndio hui hifadhi nazi kabla ya matumizi baada ya kuwa imetoka mtini kwani nazi yenyewe kwa ujumla wake una ina mafumbato mawili la kwanza hutambulika kama ni majani yake na lapili ndio kwa umaarufu kabisa hutambulika wa jina la #kifuu.

#vifuu kwa mazingira ya eatu wengi haswa kwa wale ambao ndipo minazi hupatikana huvitumia kwa mambo mbalimbali wengine huvifanya kama kuni kwa matumizi ya kupikia,kufukuzia mbu wakati wa jioni pindi kiza kinapo anza kutanda, kuondolea viroboto katika mifugo haswa kuku,na hata baadhi ya wasanii na wataalamu wa kazi za mikono hutumia kwa shughulizao kutengenezea vyombo vya matumizi ya nyumbani kama kata ama bajuli na kutengenezea mapambo ya mwilini.

#lakini hapa leo tunaendelea kujuzana matumizi ya vifuu na faida zake katika maswala ya mambo na maradhi ya kiroho kama ilivyo kawaida ya page yetu hii kwani hii haihusiani na mambo ya kisiasa wala mambo ya michezo burudani na hata utani na vichekesho.
Hapa tunajifunza mambo mbalimbali kuhusu tiba za maradhi ya mwanaadamu ya nayo tokana na maradhi ima ya kibaiologia ama maradhi ya kiroho.

#Leo kupitia kifuu tutajifunza mambo kama  yafuatayo.1-#mwenye maradhi ya kukauka ngozi.
Chukua nyama za ndani ya nazi zisage ziwe lani bila ya kutia maji changanya na mafuta ya nazi unguza vifuu mbaka viungue kabisa viponde uwe unga laini changanya na dawa mkanda wa chuma na mjafari changanya vizuri tumia kuji sugulia wilini asubuhi na jioni mbaka utakapo ona ngozi imekaa sawa.

2-#kutoa nuksi kwa mwanamke tu.

#Angalizo mwanamke huyu ahakikishe si yule mwenye nuksi ya jinni mahaba wala ame anauchawi.

#Chukua nazi ilio komaa hapa ni bora mwanamke kuikuna nazi na sii kuisaga kwa blender utaikunia kwenye sahani ya kioo changanya na majani ya mbaazi ulio komaa vizuri na maua ya mrehani hapo utanchanganya vizuri kisha utatandika nguo chini na wewe utakuwa juu na kuanzia kuji singa kama mwali kuanzia kichwani hadi unyayoni na kwauwezo wake mungu baada ya zoezi tofauti utaiyona.

3-#kumtuliza mpenzi.
#mtu anapotaka kumtuliza mpenzi wake ambaye hajatulia (kicheche)basi atachukua yai safi la kuku mweusi ataandika katika karatasi mbili tofauti moja utaandika jina lako(mtakaji) na nyingine utaandika jina la mkusudiwa (mtakiwa) utakwenda mbaka kwenye kichuguu utachimba shumo kiasi tu kisha weka karatasi yenye jina la mtakiwa chini ulifunike juu yake weka yai kisha weka karatasi ya mtakaji funika na kifuu fukia kwa manuizi juu ya yule ulie mkusudia rudi nyumbani kazi umemaliza.

4-#kuzindika nyumba.
#endapo mtu nyumbani kwake hakai kwa raha usiku mara paka wabalia hovyo ama vishindo vya ajabuajabu ama husikia kama mchanga unamwagwa juu ya paa la nyumba basi atachukua vifuu vitano (5)atachimba vishimo vitano vinne kila pembe ya nyumba na katikati ya eneo kila kifuu utamwagia mafuta ya taa na kibiritiupele na una kiwasha kwa manuizi kwamba mchawi yoyote atakapo kuja kufanya ushenzi katika eneo lile basi uone mji ule unawaka moto kama kinavyo waka kile kifuu kisha unakiwasha moto huondoki mbaka koto umalizike pale na ufukie ndio unakwenda kwenye kingine mbaka unamaliza vyote vitano hivyo hivyo.

5-#kuangamiza maadui.
Chukua kitabu cha ahlul-badir.
Kisha chukua vifuu ishirini na nane (28) kila kifuu kimoja kiandie herufi za ابجدkwa kila moja na uzani wa herufi yake kisha utasoma kila mlango wa herufi na kifuu chake mbaka yoote ishirini na nane inapokamilika  mwishoni tamalizia na baabu  رسول mara  saba (7) utaacha vifuu viungue hadi majivu kabisaa moto ukisha zimika na kupoa kabisa majivu unaweza kuya gukia ama kuyamwaga katika maji ya mto yanayo tembea. usifanyie hasira wala maonezi kwa mtu kwani usimtaje mtu jina ila nui tu mwenye kukufanyia ubaya na kutaka kukudhalilisha tu kwani ni mujarrabu ukifanya masihara dhambi ni juu yako.

6-#mapenzi. 
#unapotaka kumpagawisha mtu kimapenzi akupende mithili ya mwenda wazimu kimapenzi.
#basi chukua vifuu 21 vikwangue kwa nje kicha andika herufi za بدوح Koreza moto mkali weka chungu jikoni weka mayai ya kuku mwendu mawili (2) na lakuku mweusi  moja (1) kikipata joto panga humo vifuu vyako vyote kwenye  chungu pamoja na buni na mahindi ya njano na mtaka viache mbaka vianze kuungua kisha mwagia mafuta ya taa uviwashe moto  huku ukinuia hakika atakupenda mithili ya vile ulivyo nuia.

7-#endapo mtu anasingiziwa jambo iwe ni mtaani ama kazini na kweli jambo hilo hakulifanya.
Basi atachukua vifuu arobaini na moja (41) viandike majina ya hao watu wanao kupakazia uongo na jina la mtu anae pelekewa taarifa hizo za uongo ili akuchukie  chimba shimo kiasi washa moto ukisha kolea vizuri chukua maji ya mvua kisha uzimie moto ule kwenye lile shimo kwa manuizi ya kuzima ghadhabu na hasira za bosi ama yule ambaye anatakiwa akuchukie   ukisha zimika kabisaa fukia kwa manuizi pia nenda tulia.
Kwa maoni na ushauri piga
               +255685566362 

Wattsup +255717108210.

 Msolo rajabu yusufu.


0 comments:

Post a Comment